Tangaza Biashara yako hapa kwa bei nafuu wasilana nasi kupitia 0712 455 139 au 0687 233 209 wote mnakaribishwa. Advertise your Business here at very cheap price Contact us through +255 712 455 139 or +255 687 233 209 your all welcome.

Advertise your Business here at very cheap price Contact us through +255 712 455 139 or +255 687 233 209 your all welcome.

DR. DRE : MIMI NI BILIONEA WA KWANZA KATIKA HIP HOP, BAADA YA APPLE KUPANGA KUINUNUA KAMPUNI YAKE YA BEATS ELECTRONICS

DreRapa na Mtayarishaji wa muziki   ‘Andre Romelle Young’   maarufu kwa jina la steji Dr.Dre amesema kuwa  yeye ni bilionea wa kwanza katika Hip Hop kufuatia  kampuni ya Apple kutangaza kuinunua kampuni yake ya Beats Electronics inayotengeneza Headphones za Beats by Dre.
”Bilionea wa kwanza katika Hip Hop kutoka West Coast (alafu akatia na kionjo cha tusi)” alisema Dre katika video fupi aliyochukulia na staa wa  filamu za fast & Furious muigizaji Tyrese Gibson.
Katika Video hiyo Tyrese alikuwa akijadili kuhusiana na orodha iliyotolewa na jarida la Forbes ya wasanii wa Hip hop wanaoongoza kwa kuwa na mkwanja mrefu.
”Haiwezekani” Tyrese anasema orodha ya Forbes imebadilika ghafla” ”kwa hatua kubwa” aliongezea Dre.
Kama ilivyoripotiwa hapo jana(May08) na mtandao wa gizmodo uliosema kwamba Apple imepanga kuinunua Beats Electronics inayomilikiwa na Dre pamoja na Jimmy Iovine kwa gharama ya dola za kimarekani Bilioni 3.2 huku dola bilioni 1 zikitajwa  kuingia  mfukoni mwa mtayarishaji huyo..
Kwa mujibu wa kituo cha utangazaji cha  CNBC walisema  kwamba ununuzi huo unakwenda kinyume na sera za muanzilishi wa kapuni hiyo Steven Jobs aliyefariki Dunia mwaka 2011,  zilizokuwa zikipinga  ununuzi wa vitu vyenye gharama kubwa.
Dre anayeshikilia nafasi ya pili hivi sasa kwa wasanii wa Hip Hop wenye hela ndefu huku utajiri wake ukitajwa kufikia dola milioni 550 akiwa amemzidi Jay Z kwa tofauti ya dola milioni 30. Hiyo ni kwa mujibu wa orodha iliyotolewa na jarida la Forbes…
“I don’t really care about any of that,” “Jay Z is my guy, man. I love him to death.”  alisema Dr.Dre baada ya kupigwa swali na muandishi kuhusiana na anavyojisikia kuwa juu ya Jay Z
Tazama Video fupi hapo chini umsikilize alichosema Dre baada ya kupata shavu hilo

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...