Tangaza Biashara yako hapa kwa bei nafuu wasilana nasi kupitia 0712 455 139 au 0687 233 209 wote mnakaribishwa. Advertise your Business here at very cheap price Contact us through +255 712 455 139 or +255 687 233 209 your all welcome.

Advertise your Business here at very cheap price Contact us through +255 712 455 139 or +255 687 233 209 your all welcome.

MFUMO MPYA WA UONDOSHJI MIZIGO(TANCIS)KUONGEZA UWAZI NA UWAJIBIKAJI

 Kamishna wa Forodha na Ushuru kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Tiagi Masamaki Kabisi akiwaeleza waandishi wa Habari juu ya faida za Mfumo mpya wa Uondoshaji Mizigo bandarini(TANCIS) ikiwa unasaidia katika kufanya makadirio ya kodi sahihi kulingana na taarifa sahihi zilizoletwa kwa kutumia mfumo huo, pia utasaidia wateja kujua sehemu mizigo yao ilipo na pia wanapaswa kulipa kiasi gani kulingana na mzigo wa mteja, wakati wa Mkutano na waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam.
 Ofisa Mwandamizi wa Forodha kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Felix Tinkasimile akiwaeleza waandishi wa habari namna mfumo mpya wa uondoshaji mizingo unavyoongeza uwazi na uwajibikaji utakaosaidia kuzuia upoteaji wa mizigo bandarini ikiwemo Magari na Makontena , wakati wa Mkutano na waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Meneja wa Kituo cha Huduma cha Forodha kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Kasty Phelician akiwaeleza waandishi wa Habari majukumu ya kituo hicho ikiwemo kutoa tathnimi ya kodi unayopaswa kulipwa kwa kupitia na kuhakiki nyaraka zote kutoka kwenye kadhia zinazotumia mfumo wa TANCIS ikiwamo viwango vya ushuru wa forodha vinavyopaswa kutozwa.
 Meneja wa Forodha Bandari ya Dar es Salaam kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)Bw.Burton Kaissy akiwaeleza waandishi wa Habari namna wanavyoshirikiana na Taasisi mbalimbali kurahisisha usafirishaji wa mizigo yote inayoenda nje nchi
Baadhi ya waandishi wa Habari wakimsikiliza Meneja wa Forodha Bandari ya Dar es Salaam kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)Bw.Burton Kaissy wakati wa Ziara iliyofanyika katika mamlaka hiyo kuona jinsi mfumo wa TANCIS unavyofanya kazi.PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO.

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...