Tangaza Biashara yako hapa kwa bei nafuu wasilana nasi kupitia 0712 455 139 au 0687 233 209 wote mnakaribishwa. Advertise your Business here at very cheap price Contact us through +255 712 455 139 or +255 687 233 209 your all welcome.

Advertise your Business here at very cheap price Contact us through +255 712 455 139 or +255 687 233 209 your all welcome.

BODI MPYA YA BARAZA LA HABARI YAZINDULIWA

Jaji Kiongozi Shaban Ally Lila akihutubia katika uzinduzi wa Bodi mpya ya Baraza la Habari Tanzania kwa niaba ya Jaji Mkuu Mohamed Chande Othman kwenye Hoteli ya Blue Pearl jijini Dar es Salaam, Agosti 7,2014.
 Rais  wa Baraza la Habari aliyemaliza muda wake  Jaji Mstaafu Dk. Robert Kisanga  akihutubia katika uzinduzi wa Bodi mpya ya Baraza la Habari Tanzania ambapo alisisitiza umuhimu wa Baraza la habari na kutaka liungwe mkono kufanikisha malengo yake .Dar es Salaam, Agosti 7,2014.
 Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Kajubi Mukajanga akizungumza wakati wa kutambulisha Bodi mpya ya Baraza la Habari Tanzania kwenye Hoteli ya Blue Pearl Dar es salaam,Agosti 7,2014.
 Baadhi ya wageni waalikwa na waandishi wa habari wakiwa katika uzinduzi wa Bodi mpya ya Baraza la Habari Tanzania.

 Meneja wa Udhibiti na Viwango wa Baraza la Habari Tanzania Pili Mtambalike (Kushoto) akifuatiwa na Meneja wa Rasilimali Watu wa Baraza la Habari Tanzania Ziada Kirobo, Meneja wa Fedha wa Baraza la Habari John Nguya na Mjumbe mpya wa Bodi ya Baraza la Habari Tanzania Profesa Bernadetha Killian wakifurahia jambo wakati wa uzinduzi wa Bodi hiyo.
 Rais wa Baraza la Habari Jaji Mstaafu Thomas Mihayo akipokea cheti cha kumaliza muda wa kutumikia Bodi iliyomaliza muda wake kutoka kwa Jaji Kiongozi Shaban Ally Lila .
 Rafii Haji Makame mjumbe wa Bodi iliyomaliza muda wake akionyesha cheti alichokabidhiwa katika sherehe za kuaga bodi ya zamani na kuzindua bodi mpya ya Baraza la Habari, kulia ni Jaji Kiongozi Shaban Ally Lila na kushoto ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Kajubi Mukajanga.
Jaji Kiongozi Shaban Ally Lila akimkabidhi cheti Mjumbe wa Bodi iliyomaliza muda wake Ussu Mallya wakati wa sherehe za kuzindua Bodi Mpya na kuiaga ya zamani kwenye Hoteli ya Blue Pearl jijini Dar es salaam.
 Jaji Kiongozi Shaban Ally Lila akimkabidhi vitendea kazi Mjumbe wa Bodi mpya ya Baraza la Habari Tanzania Ndugu Badra Haji Masoud wakati wa uzinduzi wa Bodi hiyo.
Baadhi ya Wajumbe wa Bodi mpya ,wajumbe waliomaliza muda pamoja na wageni waalikwa wakifuatilia kwa makini uzinduzi wa Bodi hiyo .
 Jaji Kiongozi Shaban Ally Lila akiwa kwenye picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi mpya ya Baraza la Habari Tanzania.
Wajumbe wa Bodi Mpya na iliyomaliza muda pamoja na wageni waalikwa wakiwa katika picha ya pamoja mgeni rasmi katika uzinduzi wa bodi mpya Jaji Shaban Ally Lila (wa tatu kusoto walioketi).Picha kwa Hisani ya Adam H. Mzee wa kamerayangublog.com

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...