WADAU ARUSHA WALIMLILIA MAREHEMU WILLY
NA GLADNESS MUSHI WA FULLSHANGWE-ARUSHA
JIJI la Arusha ni moja ya mji ambao umepokea kwa masikitiko makubwa
kifo cha aliyekuwa mhariri mkuu wa gazeti la jambo leo marehemu Willy
Edward (38) aliyefariki usiku wa juni 16 ghafla kwa kusababishwa na
mshutuko wa moyo.
Kifo hiki kimesitisha wadau mbali mbali wa mtandao huu ambao walikuwa
wapenzi watembeleaji na pia hata wawakilishi wa mtandao huu kwa kuwa
kifo hicho kimetokea ghafla kwani amefariki dunia akiwa bado kijana
angali anahitajika kutoa mchango wake katika tasnia nzima ya
uahandishi wa habari.
Wakielezea kwa nyakati tofauti baadhi ya wadau mbali mbali mkoani hapa
wa jambo leo Bw. Adamu Aly alieleza kuwa kamwe hataweza kumsahau
marehemu kwa mchango wake katika tasnia ya habari kwa kuwa alikuwa
kijana mwadilifu na aliyekuwa anafanya kazi yake kwa umahiri ambapo
alikuwa hata ameipa tasnia ya uhabari sifa mbali mbali kutokana na
mawazo aliyokuwa akiyatoa.
“Marehemu Willy ni mmoja wa wahariri ambao alifanya kazi yake kwa
umakini ambapo kwa kweli inasikitisha sana kwani nimepokea msiba huu
kwa mshutuko mkubwa na huzuni nyingi kwani alikuwa kijana na bado
alikuwa anahitajika sana hasa katika kuendelea na umahiri wake wa
kazi lakini basi tu kazi ya Mungu haina makosa”alisema Adamu
Nae Qeen Lema mwandishi wa habari aliyefanya kazi na marehemu kwa
kipindi akiwa majira jioni akielezea kwa undani alivyomfahamu marehemu
alisema kuwa hatua aliyo kwa sasa amefika ni kwa ajili ya mhariri
huyo makini ambaye kila mara alikuwa akimpa
changamoto na miongozo mbalimbali kwa ajili ya kuweza kusonga mbele
zaidi kiuhandishi
kifo cha aliyekuwa mhariri mkuu wa gazeti la jambo leo marehemu Willy
Edward (38) aliyefariki usiku wa juni 16 ghafla kwa kusababishwa na
mshutuko wa moyo.
Kifo hiki kimesitisha wadau mbali mbali wa mtandao huu ambao walikuwa
wapenzi watembeleaji na pia hata wawakilishi wa mtandao huu kwa kuwa
kifo hicho kimetokea ghafla kwani amefariki dunia akiwa bado kijana
angali anahitajika kutoa mchango wake katika tasnia nzima ya
uahandishi wa habari.
Wakielezea kwa nyakati tofauti baadhi ya wadau mbali mbali mkoani hapa
wa jambo leo Bw. Adamu Aly alieleza kuwa kamwe hataweza kumsahau
marehemu kwa mchango wake katika tasnia ya habari kwa kuwa alikuwa
kijana mwadilifu na aliyekuwa anafanya kazi yake kwa umahiri ambapo
alikuwa hata ameipa tasnia ya uhabari sifa mbali mbali kutokana na
mawazo aliyokuwa akiyatoa.
“Marehemu Willy ni mmoja wa wahariri ambao alifanya kazi yake kwa
umakini ambapo kwa kweli inasikitisha sana kwani nimepokea msiba huu
kwa mshutuko mkubwa na huzuni nyingi kwani alikuwa kijana na bado
alikuwa anahitajika sana hasa katika kuendelea na umahiri wake wa
kazi lakini basi tu kazi ya Mungu haina makosa”alisema Adamu
Nae Qeen Lema mwandishi wa habari aliyefanya kazi na marehemu kwa
kipindi akiwa majira jioni akielezea kwa undani alivyomfahamu marehemu
alisema kuwa hatua aliyo kwa sasa amefika ni kwa ajili ya mhariri
huyo makini ambaye kila mara alikuwa akimpa
changamoto na miongozo mbalimbali kwa ajili ya kuweza kusonga mbele
zaidi kiuhandishi
No comments:
Post a Comment