Tangaza Biashara yako hapa kwa bei nafuu wasilana nasi kupitia 0712 455 139 au 0687 233 209 wote mnakaribishwa. Advertise your Business here at very cheap price Contact us through +255 712 455 139 or +255 687 233 209 your all welcome.

Advertise your Business here at very cheap price Contact us through +255 712 455 139 or +255 687 233 209 your all welcome.

Waziri Haroun Ali Suleiman azindua mradi wa kupunguza umasikini miongoni mwa watoto na vijana

Na Khadija Khamis –Maelezo Zanzibar
WAZIRI wa Kazi Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika Haroun Ali Suleiman ameishukuru Benki ya Maendeleo ya Áfrika( ADB) kwa kuweza kuendeleza mradi wa elimu mbadala na amali kwa awamu ya pili.

Akitoa shukrani hizo  leo huko katika Ukumbi wa Hoteli ya  Bwawani  Zanzíbar wakati akizindua mradi huo wa awamu ya pili ambao umelenga kupunguza umasikini miongoni mwa watoto na vijana ambao hawakuweza kumaliza masomo yao ya skuli  na wale ambao hawakubahatika kupata elimu kabisa .

Jumla ya sh million 23 dola za kimarekani  zimetolewa na Benki  hiyo kwa ajili ya kuendeleza  mradi  wa elimu mbadala na amali .

Waziri huyo alisema  kuwa lengo la mradi huo ni kuwapa uwezo vijana wa kujua kusoma, kuandika na kuhesabu pamoja na kuwapatia mafunzo mbali  mbali ya ujuzi ambao utawasaidia kimaisha .

 Aidha alieleza kuwa pamoja na juhudi hizo za wafadhili kazi iliyopo hivi sasa ni kutoa mashirikiano ya pamoja kwa wale wadau wa kubwa  wa Wizara tatu tofauti

Akizitaja Wizara hizo ambazo ni wadau wa elimu mjumuisho  ni Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali  ,Wizara ya Habari Utalii Utamaduni na Michezo pamoja na Wizara ya Kazi Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika .

“Kazi iliyokuwepo mbele yetu ni kubwa sana anahitaji mashirikiano kwa umoja wetu” alisema Haroun.

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...