Tangaza Biashara yako hapa kwa bei nafuu wasilana nasi kupitia 0712 455 139 au 0687 233 209 wote mnakaribishwa. Advertise your Business here at very cheap price Contact us through +255 712 455 139 or +255 687 233 209 your all welcome.

Advertise your Business here at very cheap price Contact us through +255 712 455 139 or +255 687 233 209 your all welcome.

SAFARI YA MWISHO YA MAREHEMU WILLY EDWARD LEO KATIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA

 Mchungaji akiongoza ibada ya Kuaga Mwili wa Marehemu Willy Edward leo.
 Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini,Absalom Kibanda akisoma historia fupi ya Marehemu Willy Edward wakati wa Kuaga mwili wake leo kwenye Viwanja Vya Mnazi Mmoja jijini Dar.
 Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi (CCM),Nape Nnaupe akizungumza kwenye shughuli hiyo ya kuaga Mwili wa Marehemu Willy Edward.
 Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF),Prof. Ibrahim Lipumba akitoa neno kwa wafiwa wakari wa shughuli ya Kuaga mwili wa Marehe Willy Edward leo.
 Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP,Dkt. Reginald Mengi akimpa pole Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Jambo Concepts ambao ni Wachapishaji wa Magazeti ya Jambo Leo,Juma Pinto wakati wa Shughuli ya Kuaga mwili wa Marehemu Willy Edward ambaye alikuwa ni Mhariri wa Gazeti la Jambo leo,iliyofanyika leo kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja,Jijini Dar.
 Baadhi ya Wahariri wa Vyombo mbali mbali vya Habari hapa nchini wakijiandaa kushusha jeneza lenye mwili wa Mhariri wa Gazeti la Jambo Leo,Marehemu Willy Edward Ogunde aliefariki dunia mwishoni mwa wiki mkoani Morogoro.Shughuli ya kuaga Mwili wa Marehemu Willy imefanyika leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar na baadae ikafuatia safari ya kwenda Nyumbani kwao Mara kwa Mazishi.
Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi (CCM),Nape Nnaupe akitoa heshima zake.
Bw. Athuma Hamis akitoa heshima za mwisho kwa Mwili wa Marehemu Willy Edward.
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF),Prof. Ibrahim Lipumba akitoa heshima zake za mwisho kwa Mwili wa Marehemu Willy Edward ambaye alikuwa Mhariri wa Gazeti la Jambo Leo aliefariki ghafla huko mkoani Morogoro mwishoni mwa wiki.Hafla hii ya kuaga imefanyika mchana huu katika viwanja vya Mnazi Mmoja,Jijini Dar.
Mwili wa Willy Edward ukiwekwa katika sehemu yake tayari ibada ya kuaga.
 
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini,Absalom Kibanda akibadirishana mawazo na Mkuu wa Masoko wa Benki ya NMB,Iman Kajura.
Baadhi ya Wahariri wa Vyombo Mbali mbali vya habari nchini wakiwa katika picha ya pamoja.
Ankal akiwa na Mwanalibeneke Francis Godwin
Ankal akisabahiana na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF),Prof. Ibrahim Lipumba,Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi (CCM),Nape Nnaupe pamoja na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP,Dkt. Reginald Mengi.
Mwili ukipakiwa kwenye gari tayari kwa safari ya Mara kwa Mazishi.
Waombolezaji.Picha Zote Kwa Hisani ya Michuzi Blog

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...